Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Wilaya ya Shinyanga Mjini imewahimiza viongozi na wanachama wa chama hicho
kuendelea kuimarisha umoja na mshikamano kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025,
utakaohusisha nafasi ya Rais wa Nchi, Wabunge na Madiwani.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo,
Mzee Fue Mrindoko, pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wakati wa ziara
ya kutembelea na kukagua miradi inayotekelezwa chini ya Ilani ya CCM.
Ziara hiyo imefanyika Februari 21, 2025 katika kata
za Masekelo, Ndala na Mwawaza zilizopo Jimbo la Uchaguzi Shinyanga Mjini.
Mrindoko amesema kuwa ili chama hicho kipate ushindi
wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao, ni muhimu kwa wanachama kudumisha
mshikamano na kuepuka makundi yasiyo na tija ndani ya chama.
Aidha, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya
Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, amempongeza Rais
Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuimarisha maendeleo ya nchi huku
akimhakikishia ushindi wa kishindo yeye pamoja na mgombea mwenza, Dkt. Emmanuel
Nchimbi.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bi. Doris Kibabi, amewahimiza wanachama kutoridhika na idadi ya
wanachama waliopo bali waendelee kuhamasisha wengine kujiunga.
"Tusiridhike
na wanachama tulionao, naomba tuendelee kuongeza wanachama wapya. Wanachama
hawa wasajiliwe kwa mfumo wa kielektroniki na tulipie ada za kadi zetu,"
amesema Bi. Kibabi.
Aidha, amekumbusha umuhimu wa kuendesha vikao vya
kikatiba na kikanuni ili kuimarisha chama badala ya kushughulikia migogoro
isiyo na tija.
“Tukumbuke
kuwa uhai wa chama ni kufanya vikao. Fanyeni vikao vya kikatiba na kikanuni
kwenye jumuiya zenu kwa sababu vikao vinajenga. Hali kadhalika, viongozi
mliochaguliwa naomba muongoze kama inavyotakiwa, msifanye vikao vya
kushughulikia watu, fanyeni vikao vya kujenga chama,”
amesema Kibabi.
Katika ziara hiyo, viongozi wa jumuiya wametembelea
ujenzi wa maboma mawili ya shule ya msingi Msufini B iliyopo katika mtaa wa
Mlepa, kata ya Ndala, ikiwa ni sehemu ya juhudi za CCM katika kuimarisha
miundombinu ya elimu.
Ziara hiyo inaendelea kuwa sehemu ya juhudi za CCM
katika kuimarisha chama na maendeleo ya kijamii kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka
2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza katika wa ziara
katika kata ya Masekelo, Ndala na Mwawaza.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza katika wa ziara katika kata ya Masekelo.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Zulfa Hassan akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza katika wa ziara
katika kata ya Ndala .
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza katika wa ziara katika kata ya Ndala .
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Zulfa Hassan akizungumza.
Post a Comment