Na Mapuli Kitina Misalaba
Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya
ya Shinyanga Mjini imewahimiza wakazi wa Manispaa ya Shinyanga kutumia vyema
fursa za mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Serikali kwa vikundi vya
wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Akizungumza katika ziara ya jumuiya hiyo, Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, amewasisitiza
wananchi hususan vijana kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo hiyo ili kuimarisha
maendeleo yao kiuchumi.
Ameeleza kuwa mikopo hiyo ni fursa muhimu kwa
wananchi kujiajiri na kupunguza changamoto za ajira.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, amepongeza juhudi za Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuboresha
huduma za jamii na kutoa fursa za kiuchumi kwa wananchi ikiwa ni pamoja na mikopo
hiyo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi, amesisitiza umuhimu wa kuongeza wanachama wapya
ndani ya CCM, akisema kuwa chama kinahitaji nguvu mpya na watu wenye ari ya
kuchangia maendeleo.
“Tunahamasisha
wanachama wapya kujiunga na Jumuiya ya Wazazi ili kushiriki katika shughuli za
maendeleo na kujifunza masuala muhimu ya kijamii, ikiwemo malezi bora na ujenzi
wa familia imara,” amesema Doris.
Naye Diwani wa Kata ya Chamaguha ambaye pia ni
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, amesisitiza umuhimu wa mikopo hiyo kwa
maendeleo ya vijana, akiwataka kujipanga na kuunda vikundi vyenye malengo
mahsusi ili waweze kunufaika na fursa hiyo.
Ameongeza kuwa Serikali inatekeleza miradi
mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya barabara, afya,
elimu na maji, hivyo ni jukumu la wananchi kushirikiana kwa karibu na Serikali
ili kunufaika na juhudi hizo.
Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini
imehitimisha ziara yake ya kutembelea kila kata ndani ya Manispaa ya Shinyanga,
ambapo leo wamefika katika Kata ya Kolandoto, Ibadakuli na Chamaguha.
Katika ziara hiyo, viongozi hao wametembelea na
kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika kata hizo, huku
wakihimiza uzalendo, mshikamano na kuendelea kuiunga mkono CCM kwa kazi
inayofanywa katika kuboresha maisha ya wananchi.
Ziara hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
chama akiwemo Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini,
Mhandisi James Jumbe, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya hiyo, Bi. Doris Yotham
Kibabi, pamoja na wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini ambao ni Daniel Kapaya, Mwalimu Giti Boniphace, Mary Makamba,
Zulfa Hassan pamoja na Katibu wa Elimu na Malezi wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Richard Mseti.
Aidha, jumuiya hiyo imetoa elimu kuhusu lishe bora,
malezi, ukatili wa kijinsia na umuhimu wa wanachama wapya kujisajili ndani ya
CCM.
Baadhi ya wanachama walioshiriki katika ziara hiyo
wamepongeza juhudi za Jumuiya ya Wazazi kwa kutoa elimu juu ya masuala ya lishe,
malezi na ukatili wa kijinsia, wakisema kuwa elimu hiyo itasaidia katika
kuboresha maisha yao ya kila siku.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Mary Makamba akizungumza.
Katibu wa Elimu na Malezi wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Richard Mseti akizungumza katika kata ya Kolandoto.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Zulfa Hassan akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Daniel Kapaya akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mwalimu Giti Boniphace akizungumza.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Yotham Kibabi akiwahamasisha wanachama na viongozi kulipa ada
kwa wakati na kuendelea kuongeza wanachama wapya.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Yotham Kibabi akiwahamasisha wanachama na viongozi kulipa ada
kwa wakati na kuendelea kuongeza wanachama wapya.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Yotham Kibabi akiwahamasisha wanachama na viongozi kulipa ada
kwa wakati na kuendelea kuongeza wanachama wapya.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Zulfa Hassan akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mwalimu Giti Boniphace akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Daniel Kapaya akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi. Mary Makamba akizungumza.
Katibu wa Elimu na Malezi wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Richard Mseti akizungumza katiika kata ya Chamaguha.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Yotham Kibabi akiwahamasisha wanachama na viongozi kulipa ada
kwa wakati na kuendelea kuongeza wanachama wapya.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Yotham Kibabi akiwahamasisha wanachama na viongozi kulipa ada
kwa wakati na kuendelea kuongeza wanachama wapya.
Post a Comment