Katibu tawala wa Mkoa wa Shinyanga
CP. Salum Hamduni akizundua Bodi Mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Shinyanga leo Februari 11, 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamdui,
ameisisitiza Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga
kutekeleza majukumu yake kwa weledi, ikiwemo kuisimamia menejimenti ya
hospitali katika utekelezaji wa majukumu yake.
Amebainisha kuwa menejimenti hiyo inawajibika moja
kwa moja kwa bodi, huku Mganga Mfawidhi wa hospitali akihudumu kama Katibu wa
Bodi.
CP Hamdui ametoa wito huo leo Februari 11, 2025,
wakati akizindua rasmi bodi hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na
kwamba hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Vigmark Hotel,
ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na wadau wa sekta ya afya.
Hamdui amesema bodi inapaswa kukutana mara nne kwa
mwaka, kila mwisho wa robo ya mwaka, ili kupitia na kuidhinisha au kukataa
taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Hospitali ambapo pia bodi inaweza
kuitisha mikutano ya dharura kushughulikia masuala yenye athari katika utoaji
wa huduma.
Aidha, bodi inawajibika kupitia maombi ya
marekebisho ya bei za huduma za afya kwa kushirikisha wadau na kuzingatia
miongozo, sheria, kanuni, na taratibu za nchi kabla ya kuwasilisha mapendekezo
kwa Waziri mwenye dhamana.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, aliyemwakilisha
Mkuu wa Mkoa, akisoma hotuba iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa, amewapongeza
wajumbe wa bodi kwa kuteuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Afya ambapo amesisitiza
kuwa bodi hiyo ni chombo muhimu katika uendeshaji wa huduma za afya katika Hospitali
za mikoa.
“Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ni kiungo muhimu kati ya wananchi na
serikali yao katika kusimamia utoaji wa huduma bora za afya,”
amesema Katibu Tawala wa Mkoa.
Ameeleza kuwa Sera ya Afya ya mwaka 2007, kipengele
cha 8.2, pamoja na Mwongozo wa Usimamizi wa Shughuli za Afya katika ngazi za
mkoa wa mwaka 2019, vinaeleza umuhimu wa bodi za ushauri za hospitali za rufaa
katika kuhakikisha uwazi na ushirikishwaji wa jamii katika utoaji wa huduma za
afya.
Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Luzila John, ametoa taarifa kuhusu Hospitali
hiyo, akieleza historia na maendeleo yake tangu ilipoanzishwa mwaka 1947 baada
ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Amesema Hospitali hiyo ilipandishwa hadhi kuwa
Hospitali ya Mkoa mwaka 1974 na kutangazwa rasmi kuwa Hospitali ya Rufaa ya
Mkoa mwaka 2010 ambapo tangu mwaka 2022, Hospitali imekuwa ikitoa huduma katika
eneo jipya lililopo Kata ya Mwawaza.
Dkt. Luzila amesema Hospitali hiyo inatoa huduma
mbalimbali kwa wagonjwa wa nje na ndani, ikiwa ni pamoja na huduma za kibingwa
za afya ya akina mama, watoto, upasuaji, magonjwa ya ndani, na huduma za
dharura.
Kwa mwaka uliopita, hospitali ilihudumia wagonjwa wa
nje 58,319 na wagonjwa waliolazwa 6,787ambapo akinamama 1,421 walijifungua
hospitalini hapo, huku 802 wakifanyiwa upasuaji.
Amebainisha kuwa Hospitali hiyo imeendelea kuboresha
huduma zake kwa kushirikiana na madaktari bingwa pamoja na kutumia mfumo wa
huduma mkoba ili kuwafikia wananchi kwa urahisi.
Dkt. Luzila ameainisha changamoto mbalimbali
zinazoikabili hospitali hiyo, ikiwa ni pamoja na upungufu wa miundombinu ya
majengo ili kutoa huduma zote zinazohitajika na ubovu wa barabara zinazoelekea
Hospitalini, jambo linalosababisha usumbufu kwa wagonjwa, hasa wale mahututi na
waliovunjika mifupa.
Ameomba serikali iendelee kusaidia katika ujenzi wa
miundombinu na kuboresha huduma za afya, huku akitoa shukrani kwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mchango
wake mkubwa katika sekta ya afya.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yudas
Ndungile, amesisitiza kuwa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii, na Lishe ya Mkoa ina
jukumu la kusimamia na kuratibu huduma za afya.
Amesema Hospitali hiyo ina wataalamu wa afya
wabobezi wanaosaidia kuhakikisha huduma za kibingwa zinapatikana kwa wananchi.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya
ushauri ya Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. John Majigwa,
akizungumza kwa niaba ya bodi, amesema:
“Sisi
kama bodi tunapenda kuahidi kuwa tutafanya kwa uwezo wetu, kwa nguvu zetu na
kwa upendo ili tuweze kuinua huduma za afya katika mkoa wetu. Bodi hii itafanya
kazi kwa ushirikiano na watumishi wote, ngazi ya jamii na mkoa kwa ujumla, kwa
sababu lengo letu ni kusaidia kuinua huduma za afya katika mkoa wetu ili kila
mmoja aweze kufaidika na huduma hizi.”amesema Dkt. Majigwa
Uzinduzi wa bodi hiyo unatarajiwa kusaidia kuboresha
huduma za afya katika Mkoa wa Shinyanga kwa kuhakikisha usimamizi mzuri wa
hospitali na kushirikisha jamii katika maamuzi yanayohusu huduma za afya.
Katibu tawala wa Mkoa wa Shinyanga
CP. Salum Hamduni akizundua Bodi Mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Shinyanga leo Februari 11, 2025.
Katibu tawala wa Mkoa wa Shinyanga
CP. Salum Hamduni akizundua Bodi Mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Shinyanga leo Februari 11, 2025.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt.Yudas
Ndugile akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wa Shinyanga.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt.Yudas
Ndugile akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wa Shinyanga.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt.Luzila John akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi
mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt.Luzila John akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi
mpya ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi mpya ya
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dk.John Majigwa akiahidi kuwa bodi hiyo
itatekeleza majukumu yake kwa weledi.
Mwakilishi wa Wizara ya Afya
Dk.Fadhili Kibaya akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi mpya ya Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Viongozi mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa Bodi
ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Februari 11, 2025.
Viongozi mbalimbali
Post a Comment