Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya CCM wilayani humo Mhandisi James Jumbe akizungumza.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mjumbe wa
Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye
pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya CCM wilayani humo Mhandisi James
Jumbe, amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amefanikisha maendeleo makubwa katika
kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.
Akizungumza katika ziara ya Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga mjini, Mhandisi Jumbe ameeleza kuwa maendeleo haya
yameonekana katika sekta mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Daraja la Busisi, reli ya
kisasa ya SGR, viwanda, miundombinu, afya, mahusiano ya kimataifa, ukuaji wa
uchumi, na usuluhishi wa migogoro.
“Rais
Samia ameonesha uzalendo wa hali ya juu katika kusukuma maendeleo ya nchi yetu.
Tumeshuhudia utekelezaji wa miradi mikubwa kama Bwawa la Mwalimu Nyerere,
ambayo siyo tu inahitaji rasilimali kubwa bali pia inahitaji ujuzi wa hali ya
juu kuitekeleza kwa mafanikio,” amesema Mhandisi
Jumbe.
Ameongeza kuwa katika suala la ukusanyaji wa mapato
na kodi, serikali ya Rais Samia imefanikiwa kuimarisha mifumo, hali ambayo
imeongeza mapato ya taifa na kuwezesha utekelezaji wa miradi mikubwa kwa
wakati.
“Kasi
ya maendeleo ni kubwa na hakuna mradi uliokwama licha ya changamoto mbalimbali.
Mama Samia ameonesha kuwa ni kiongozi mwenye maono, uwezo wa kusimamia miradi,
na anatekeleza mipango yake kwa kasi kubwa kwa manufaa ya wananchi wote,”
amesema Jumbe.
Mhandisi Jumbe amewahamasisha wanachama wa CCM na
wananchi kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Rais Samia pamoja na mgombea
mwenza wake Dkt. Emmanuel Nchimbi, akibainisha kuwa ni viongozi makini wenye
uwezo mkubwa wa kusimamia maendeleo ya nchi.
“Kama
chama, tumepewa wagombea makini. Dkt. Emmanuel Nchimbi ni mbobezi katika
uongozi, siasa na mahusiano ya kimataifa, na Dkt. Hussein Mwinyi ameleta
maendeleo makubwa Zanzibar. Kwa hiyo, ni wakati wa kuendelea kuwaunga mkono
viongozi hawa,” amesemaJumbe.
Aidha Mhandisi James Jumbe Wiswa pia amekabidhi
mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Kituo cha Afya
Kambarage, Manispaa ya Shinyanga.
Mchango huo unalenga
kuimarisha usalama wa wagonjwa, hususan akina mama na watoto wachanga
wanaopatiwa huduma katika kituo hicho.
Akizungumza wakati wa makabidhiano, Mhandisi Jumbe
amesema ametoa msaada huo kama sehemu ya kutimiza ahadi yake ya kuunga mkono
juhudi za Serikali za kuboresha sekta ya afya.
"Nimeamua
kutimiza ahadi yangu ya kusaidia ujenzi wa uzio wa Kituo cha Afya Kambarage ili
kuhakikisha mazingira salama kwa wagonjwa, hususan akina mama na watoto
wanaopata huduma hapa. Kamati ya Kituo hiki ilileta ombi, nami nikaona ni
muhimu kulitekeleza kwa vitendo," amesema Mhandisi
Jumbe.
Ameeleza kuwa mchango
huo ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kuboresha
sekta ya afya kwa kuhakikisha vituo vya afya vinakuwa na miundombinu bora na
salama.
“Rais
Samia amejitahidi kuimarisha sekta ya afya kwa kuleta vifaa tiba vya kisasa na
kuboresha huduma. Sisi kama wadau wa maendeleo tunapaswa kushiriki katika
kuunga mkono juhudi hizi. Nawaomba wafanyabiashara wa Shinyanga pia waone
umuhimu wa kuchangia miradi ya maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake,
Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Afya Kambarage, Adolf Nzwanzungwanko,
ameushukuru mchango huo na kueleza kuwa utasaidia kuimarisha usalama wa kituo
hicho, hususan nyakati za usiku.
Naye Mganga Mfawidhi wa
Kituo hicho, Dkt. Ernest Magula, amesema ujenzi wa uzio huo utaongeza ufanisi
katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa na kupunguza changamoto ya watu wasiokuwa
na mahitaji ya kitabibu kuzurura ndani ya eneo la hospitali.
Katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi
ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, pamoja na mambo mengine ameahidi
kuwa jumuiya hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi zote za maendeleo
zinazotekelezwa chini ya Ilani ya CCM.
Naye Katibu wa Jumuiya hiyo, Bi Doris Yotham Kibabi,
amewahamasisha viongozi wa jumuiya hiyo katika ngazi za kata, matawi na mashina
kuongeza wanachama wapya ili kukiimarisha chama.
Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini
leo Februari 22, 2025 imefanya ziara zake katika kata za Kambarage, Lubaga, na
Mjini kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza
mshikamano miongoni mwa wanachama.
Post a Comment