TAZAMA VIDEO
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mashine ya kusaga unga inayomilikiwa na Mzee Joseph
Pombe katika Kijiji cha Ipeja, Kata ya Itilima, Halmashauri ya Wilaya ya
Kishapu, imeungua moto na kuteketeza kila kitu kilichokuwemo ndani baada ya
hitilafu ya umeme.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ipeja, Jackson Mwabila,
amesema tukio hilo limetokea Februari 24, 2025, ambapo moto huo ulianza ghafla
na kusababisha hasara kubwa.
“Tarehe
24, 2, 2025 lilitokea tukio kwenye kijiji changu, kuna mashine ya kusaga unga
ilitokea hitilafu ya umeme, moto ukalipuka na kuwasha nyumba yote. Yaani mpaka
sasa ninavyoongea, nyumba imeteketea kabisa,” amesema
Mwabila.
Ameeleza kuwa mashine tatu zilikuwepo ndani ya jengo
hilo, ikiwemo mashine ya kusagia unga, mashine ya kukoboa mahindi na mashine ya
kukoboa mpunga, lakini vyote vimeteketea kwa moto huo.
“Jitihada
za kuuzima moto zilifanyika, tuliwapigia simu lakini waliwasili kwa kuchelewa.
Walifanikiwa kuuzima moto huo lakini vifaa vyote vilikuwa tayari vimeteketea,”
ameongeza Mwenyekiti huyo.
Pamoja na mashine hizo, ndani ya jengo kulikuwa na
mahindi ya kusaga, mpunga, na bidhaa nyingine mbalimbali ambazo zote
zimeangamia kutokana na moto huo.
Post a Comment