Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono akizungumza.
Na Daniel Sibu, Misalaba Media
Kulikuwa na nyimbo za shangwe, tarumbeta, na mabango yaliyomsifu Mungu kwa kumpa kanisa kiongozi mpya wa kiroho.ASKOFU MTEULE DKT. MONO: “SIKUTEGEMEA MAPOKEZI KAMA HAYA”
"Kwa kweli leo nimetekewa kwa sababu sikujua kama kuna jambo la namna hii. Nimekutana na jambo ambalo sikulitegemea kabisa. Nimeona magari, watu, na tarumbeta ambapo nilijikuta nikitekewa," alisema kwa furaha.
"Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa yote aliyotenda. Ametembea nami katika utumishi wake, na sasa amenipa nafasi nyingine kubwa ya kulitumikia kanisa lake katika Dayosisi ya Mwanga," alisema Dkt. Mono.
Pia alitoa shukrani za dhati kwa Askofu wa KKKT DKMZV, Mchungaji Dkt. Yohana Ernest Nzelu, kwa ushirikiano wake katika utumishi".
"Ni haki yetu kama Dayosisi kumshukuru Mungu kwa ajili ya nafasi hii aliyopewa Dkt. Mono. Tunampongeza kwa dhati na tunamtakia kila la heri katika utumishi wake mpya Dayosisi ya Mwanga," alisema Askofu Nzelu.
Aliendelea kueleza kuwa uongozi wa KKKT DKMZV utatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuwa mchakato wa kuhama kwa Dkt. Mono unafanyika kwa utaratibu mzuri na kwa utukufu wa Mungu.HISTORIA YA DKT.
MONO NA SAFARI YAKE
YA KIROHO
Dkt. Daniel Henry Mono amekuwa
Msaidizi wa Askofu wa KKKT DKMZV, akifanya kazi kwa karibu na Askofu Nzelu katika
kuimarisha kanisa. Mnamo Machi 10, 2025, akiwa nchini Burundi kwa majukumu ya
kikazi, alichaguliwa kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga kupitia Mkutano Mkuu wa
Dayosisi hiyo uliofanyika katika Kanisa Kuu la Mwanga.
Kiti cha Askofu wa Dayosisi ya Mwanga kilikuwa wazi baada ya kifo cha aliyekuwa Askofu wa kwanza wa Dayosisi hiyo, Hayati Askofu Chediel Sendoro, aliyefariki dunia Septemba 9, 2024, kwa ajali ya gari huko Kisangiro, Mwanga.HITIMISHO
Mapokezi haya makubwa yanaonesha jinsi KKKT DKMZV inavyothamini viongozi wake na jinsi waumini wanavyoonyesha upendo kwa watumishi wa Mungu. Safari ya Dkt. Mono sasa inahamia Mwanga, ambako anatarajiwa kuanza utumishi wake rasmi kama Askofu wa Dayosisi hiyo.
Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono akizungumza baada ya kuwasili.













Post a Comment