
Na Mapuli Kitina Misalaba
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,
Stephen Wasira, amesema kuwa chama hicho hakina mpango wa kuondoka madarakani
kwa sababu kimeendelea kuwa nguzo ya amani na maendeleo ya Tanzania.
Wasira ametoa kauli hiyo leo Machi 27, 2025, wakati
wa mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Kahama, ambapo ameeleza kuwa CCM
kimekuwa kikitatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi, huku
maendeleo makubwa yakishuhudiwa hasa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi
wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
"CCM ni chama kilichounganisha vyama vilivyoleta ukombozi Tanzania
na Afrika. Tumejenga umoja wa kitaifa kwa makabila yote, hatujawahi kupigana
wenyewe kwa wenyewe, tunasuluhisha migogoro ya mataifa mengine na kupokea
wakimbizi wakati nchi nyingine zinapigana. Vyama vidogo haviwezi kujilinganisha
nasi. Hatutoki madarakani kwa sababu wananchi wanatuunga mkono na maendeleo
yanaonekana," amesema Wasira.
Akizungumzia maendeleo yaliyofanikishwa na Rais
Samia, Wasira amebainisha kuwa miradi mikubwa iliyoanzishwa na Hayati John
Magufuli imeendelea kwa kasi kubwa chini ya uongozi wa Rais wa awamu ya sita.
"SGR iliyoanzishwa na Magufuli sasa imekamilika kwa kipande cha Dar
es Salaam – Morogoro, na inaendelea kujengwa hadi Mwanza kupitia Isaka, Kahama.
Bwawa la umeme la Julius Nyerere lilikuwa asilimia 30 Magufuli alipofariki,
sasa limefikia asilimia 70 na tayari tunaumeme wa mradi huo. Daraja la Busisi
pia limeendelea kujengwa na sasa liko zaidi ya asilimia 60 ya utekelezaji
wake," amesema Wasira.
Katika mkutano huo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
Taifa kutoka Mkoa wa Shinyanga, Gasper Kileo (GAKI), ameeleza kuwa Shinyanga
itaendelea kuwa ngome ya CCM na kuhakikisha ushindi wa kishindo katika uchaguzi
mkuu wa 2025.
"Shinyanga tulikuwa nafasi ya pili kwa kura nyingi mwaka 2020,
lakini 2025 tutakuwa wa kwanza. Rais wetu Dkt. Samia na mgombea mwenza wake
Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi tutawapatia kura za kutosha,"
amesema Kileo.
Aidha, Wajumbe wengine wa Halmashauri kuu ya CCM
Taifa wamewataka wanachama wa CCM kuendelea kushikamana na kuwatumikia wananchi
kwa kutatua changamoto mbalimbali za kijamii.
Pia, wamelaani
tukio la kudaiwa kushambuliwa kwa mwenezi wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA
(BAWACHA) Taifa, Bi. Sigrada Mligo, wakimtaka Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa kutoa
tamko rasmi kuhusu tukio hilo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala
Mlolwa, ameeleza changamoto mbalimbali zinazowakabili wachimbaji wadogo wa
madini wilayani Kahama, huku akiomba ziweze kushughulikiwa ambapo Wasira ametoa
maagizo kwamba wachimbaji hao wasisumbuliwe na akaahidi kuwa changamoto zao
zitatatuliwa.
Wakati huo huo, amebainisha kuwa changamoto za kodi
kwa wafanyabiashara pia zitashughulikiwa.
Katika hatua nyingine, Mbunge wa Jimbo la Ushetu,
Mhe. Emmanuel Cherehani, ameiomba Serikali kuongeza idadi ya mameneja wa TARURA ili kila Halmashauri katika Wilaya ya Kahama iwe na Menaja kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa miradi ya barabara.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,
Stephen Wasira, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara uliofanyika wilayani
Kahama leo Machi 27, 2025.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,
Stephen Wasira, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara uliofanyika wilayani
Kahama leo Machi 27, 2025.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa
wa Shinyanga, Gasper Kileo (GAKI), akizungumza kwenye mkutano huo wa hadhara Wilaya
ya Kahama leo Machi 27, 2025.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala
Mlolwa, akieleza changamoto za wachimbaji wadogo wa madini.
Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani, akizungumza
kwenye mkutano huo wa hadhara Wilaya ya Kahama leo Machi 27, 2025.
Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani, akizungumza
kwenye mkutano huo wa hadhara Wilaya ya Kahama leo Machi 27, 2025.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Awali Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Bara, Stephen Wasira,akiwasili katika mkutano wa hadhara Wilaya ya kahama
ambapo ameongeza na viongozi mbalimbali.
Post a Comment