" KAMPENI YA MTI WANGU BIRTHDAY YANGU YAFIKISHA MITI MIL 4.8

KAMPENI YA MTI WANGU BIRTHDAY YANGU YAFIKISHA MITI MIL 4.8

Na Halima Issa Hassani, Misalaba Media

Rai imetolewa kwa Wakazi wa Dodoma kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu zoezi la kupanda miti  ili kusaidia utunzaji wa Mazingira na kuendelea kupambana na mabadiliko ya Tabianchi, kwani mbinu ya kukabiliana na hali hiyo ni kupanda miti kwa wingi.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala msaidizi Sekta za Uchuni na Uzalishaji Mkoa wa Dodoma Bi.Aziza Mumba Machi, 2025 Jijini Dodoma mara baada ya kumalizika kwa zoezi la upandaji miti ya Kampeni inayosema Mti wangu,Birthday yangu inayoratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma katika eneo la wazi la ukanda wa kijani, Nanenane kata ya Nzuguni.

Aidha Bi. Aziza ameongeza kuwa tangu walipoanza kampeni hii ya Mti wangu,Birthday yangu wamekwisha kupanda miti takribani Milioni 4 na laki 8 na sio kupanda tu bali hata katika kuendelea kuitunza ili watu wajue kuwa mti ukiutunza unakua vizuri.

Kampeni hii ya mti wangu,Birthday yangu imeasisiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bwana Gaspar Mmuya kwa kupanda miti kwenye siku za kuzaliwa ambayo hufanywa kila tarehe 18 ya mwezi.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post