Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa
Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025, amefuturisha viongozi wa dini,
waumini, na wananchi wa Shinyanga, huku akisisitiza mshikamano na maombi kwa
taifa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Hafla hiyo imefanyika mjini Shinyanga, ikiambatana
na dua maalum iliyoongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya,
ambapo maombi yameelekezwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Samia Suluhu Hassan, maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, amani ya taifa,
pamoja na ustawi wa jamii kwa ujumla.
Katika dua hiyo, Sheikh Makusanya pia amemwombea
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, akimuomba Mwenyezi Mungu
aendelee kumbariki, kumlinda, na kumpa nafasi ya juu zaidi katika majukumu yake
ya uongozi.
“Katika
kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa
Ramadhani, tunapaswa kutafakari umuhimu wa maombi kwa viongozi wetu na
taifa kwa ujumla, tukiamini kwamba baraka za Mwenyezi Mungu zinaweza kuleta
mwelekeo mzuri katika hatima ya nchi yetu”.amesema Sheikh
Makusanya
Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu wa CCM Mkoa wa
Shinyanga, Odilia Batimayo, amewashukuru viongozi wa dini kwa ushirikiano wao
na kuwaomba waendelee kudumisha mshikamano, hasa katika kipindi hiki
kinachoelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Pia ameahidi kuwa chama hicho kitaendelea
kushirikiana nao kwa karibu ili kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea
kutawala.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
dini, wakiwemo:
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategile, Maimamu
na Masheikh wa Kata (BAKWATA), Wajumbe wa Baraza la Halmashauri Kuu (BAKWATA)
Mkoa wa Shinyanga, Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu (JUWAKITA) Mkoa wa Shinyanga,
Taasisi ya Istiqama, MDB, Isuwat, Zawiya, JUVIKIBA Wilaya ya Shinyanga, Wazee
wa dini na viongozi wa taasisi za Kiislamu
Viongozi mbalimbali wa Dini akiwepo Sheikh wa Mkoa
wa Shinyanga Ismail Makusanya wakichukua Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi mbalimbali wa Dini akiwepo Sheikh wa Mkoa
wa Shinyanga Ismail Makusanya wakichukua Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategile, akichukua
Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa
Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi mbalimbali wa JUWAKITA Shinyanga akichukua Futari
ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Odilia
Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi mbalimbali wa JUWAKITA Shinyanga akichukua Futari
ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Odilia
Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi mbalimbali wa JUWAKITA Shinyanga akichukua Futari
ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Odilia
Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi wa dini, waumini, na wananchi wa Shinyanga,
wakichukua Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi wa dini, waumini, na wananchi wa Shinyanga,
wakichukua Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Viongozi wa dini, waumini, na wananchi wa Shinyanga,
wakichukua Futari ambayo imeandaliwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo, Machi 28, 2025.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, akisoma
Dua maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu
Hassan, maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, amani ya taifa, pamoja na ustawi
wa jamii kwa ujumla.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, akisoma
Dua maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu
Hassan, maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, amani ya taifa, pamoja na ustawi
wa jamii kwa ujumla.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, akisoma
Dua maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu
Hassan, maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, amani ya taifa, pamoja na ustawi
wa jamii kwa ujumla.
Post a Comment