" MILION 225,879,500 KUTOLEWA KWA VIKUNDI VILIVYOKIDHI VIGEZO MIKOPO YA ASILIMIA 10 MANISPAA YA SHINYANGA

MILION 225,879,500 KUTOLEWA KWA VIKUNDI VILIVYOKIDHI VIGEZO MIKOPO YA ASILIMIA 10 MANISPAA YA SHINYANGA


Na:Mwandishi wetu SHINYANGA

Katika Kuhakikisha jamii inaondokana na umasikini na kujikwamua kiuchumi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imetoa mafunzo kwa jumla ya vikundi (19) vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, vikundi vilivyokidhi kupata mkopo wa asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kupitia mapato ya ndani  mikopo isiyo na riba.

 

Akizungumza leo Machi, 22,2025 Katika Mafunzo haya Afisa maendeleo ya jamii kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Bi. Nyanjula Kiyenze amesema jumla ya Tsh. Milion 225,879,500/= zimetengwa kwa  ajili ya vikundi hivyo ambapo Kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2024 inatutaka kabla ya vikundi vilivyokidhi kupata mkopo havijapokea ni lazima vipate mafunzo ili kuongeza uelewa juu ya mkopo huo.

 "jumla ya Tsh milion  225,879,500/= ambapo vikundi vya wanawake ni Tsh 127,927,500/= vikundi vya vijana Milion 123,952,000/= na Mtu mwenye ulemavu ni Tsh4,000,000/= zimetolewa na Halmashauri mikopo ya asilimia kumi isiyokuwa na riba  ili vikundi hivi viweze kujikwamua kiuchumi". Amesema Bi. Nyanjula.

 Awali akifungua mafunzo haya Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Masumbuko amevisisitiza vikundi hivyo kuwa na nidhamu ya Fedha, kuwa waaminifu Katika kurejesha mikopo hiyo ili iweze kuwanufaisha wananchi wengine.

 "Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inafanya kila liwezekanalo Kuhakikisha makundi haya yanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini, Fedha hizi ni mapato ya ndani ambayo ni Kodi za wananchi, sasa niombe kuwa na nidhamu ya Fedha hizi, kuweni waaminifu Katika kurejeshe ili vikundi vingine navyo vipate kama ninyi mlivyopata. Amesema". Mhe Masumbuko

 

Katika vikundi hivyo jumla ya mada (5) zimefundishwa Usimamizi wa vikundi, Utatuzi wa migogoro, Usimamizi wa biashara, Utunzaji wa kumbukumbu pamoja  na Msaada wa kisheria (MSLAC) zimefundishwa kwa vikundi 19 kutoka kata 9 kati ya Kata 17 za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga zilizokidhi kupata mkopo huo.

Msitahiki meya wa Halmashauri ya manispaa ya shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akifungua mafunzo kwa vikundi vilivyokidhi kupata mkopo wa asilimia kumi (4:4:2) kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu 

Afisa Maendeleo ya jamii Halmashauri ya manispaa ya shinyanga Bi. Nyanjula Kisenye akitoa mafunzo ya mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. vilivyokidhi kipewa mkopo huo.

Afisa kutoka kitengo cha msaada wa kisheria (Mama Samia legal Aid Campaign) Halmashauri ya manispaa ya shinyanga Bi. Omana Joseph akitoa mafunzo ya msaada wa kisheria katika mafunzo hayo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


vikundi vilivyokidhi kupata mkopo wa asilimia kumi vikisikiliza mafunzo inayotolewa na halmashauri bila riba


vikundi vilivyokidhi kupata mkopo wa asilimia kumi vikisikiliza mafunzo inayotolewa na halmashauri bila riba

Afisa Maendeleo ya jamii Halmashauri ya manispaa ya shinyanga Bi.Wema Mashaka ambaye pia ni afisa malalamiko akitoa mafunzo juu ya maada ya migogoro  kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. vilivyokidhi kupewa mkopo huo.












 

Post a Comment

Previous Post Next Post