" MISA-TAN YAPATA WAFADHILI KWA AJILI YA WADAU SUMMIT 2025

MISA-TAN YAPATA WAFADHILI KWA AJILI YA WADAU SUMMIT 2025

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mkutano wa MISA-TAN na wadau (MISA-TAN - Wadau Summit 2025) unaotarajiwa kufanyika Machi 14, 2025, jijini Dodoma, umeendelea kupata msukumo baada ya taasisi mbalimbali kuthibitisha kushiriki kama wafadhili wa kongamano hilo.

Mkutano huo unaoandaliwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), utawakutanisha waandishi wa habari na wadau wa sekta ya habari na mawasiliano ili kujadili masuala muhimu yanayohusu uhuru wa vyombo vya habari, maendeleo ya sekta hiyo, na ushirikiano baina ya wadau.

Miongoni mwa taasisi zilizojitokeza kufadhili mkutano huo ni Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB).

Taasisi nyingine ni Shirika la TASHICO, Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC), na Pan-African Constructive Journalism Initiative (PACJI). Ushiriki wa taasisi hizo unatarajiwa kuleta mchango mkubwa katika kufanikisha kongamano hilo na kujenga mazingira bora ya tasnia ya habari nchini.

Mkutano huo utakuwa na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule.


Post a Comment

Previous Post Next Post