Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili
Julius Mtatiro, akifungua mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga leo Machi 21, 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro,
amewataka walimu kuzingatia misingi na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa
majukumu yao.
Akizungumza
katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya Shinyanga, pamoja na mambo
mengine DC Mtatiro amewahimiza walimu kujiepusha na mikopo yenye riba kubwa
ambayo mara nyingi husababisha migogoro sehemu za kazi.
Amesisitiza kuwa walimu wanapaswa kuwa makini katika
masuala ya kifedha ili kuepuka matatizo yanayoweza kuathiri utendaji wao wa
kazi.
Aidha, ameendelea kuwasisitiza walimu kujenga tabia
ya kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuimarisha afya zao na kuepukana na
magonjwa yanayotokana na ukosefu wa mazoezi, kama vile shinikizo la damu na
kisukari.
Katibu wa CWT Wilaya ya Shinyanga, Rose Mboneko,
akisoma risala kwa mgeni rasmi, ameeleza kuwa chama hicho kitaendelea
kutekeleza majukumu yake kwa weledi.
Amesema miongoni mwa majukumu hayo ni kufundisha
wanafunzi, kutetea maslahi ya walimu, kushiriki kazi mbalimbali za kitaifa,
kutoa huduma za kisheria kwa wanachama, kuwahamasisha walimu kujiendeleza
kitaaluma, na kuhimiza ufaulu wa wanafunzi.
Hata hivyo, Mboneko ametaja changamoto zinazowakabili
walimu, zikiwemo Madeni ya mshahara na yasiyo ya mshahara kutolipwa kwa wakati,
Upungufu wa nyumba za walimu, Ukosefu wa mafunzo ya kutosha kuhusu mitaala
mipya, Upungufu wa walimu katika baadhi ya shule pamoja na Vikokotoo visivyo
rafiki kwa walimu wastaafu.
Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Wanawake CWT
Wilaya ya Shinyanga Rose Mabana amesoma taarifa ya utendaji wa chama kwa
kipindi cha miaka miwili na nusu, kuanzia Oktoba 2022 hadi Machi 2025.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa chama kimefanikiwa
kutekeleza malengo yake, ikiwa ni pamoja na Uboreshaji wa huduma kwa wanachama,
Usajili wa wanachama wapya, Ufuatiliaji wa madeni ya mishahara na yasiyo ya
mishahara ambapo serikali imeendelea kulipa madeni hayo, Kutoa elimu ya
wafanyakazi kwa walimu mahala pa kazi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wilaya ya Shinyanga ina walimu
wa shule za msingi na sekondari jumla ya 1,064, ambapo wanachama wa CWT ni 945.
Walimu wasiokuwa wanachama ni 119, huku idadi ya walimu wanaume ikiwa 458 na
wanawake 606.
Mkutano huo pia umehusisha uchaguzi wa viongozi mbalimbali
wa chama, wakiwemo Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Shinyanga pamoja na wawakilishi
wa shule za msingi na sekondari. Uchaguzi huo ni sehemu ya utaratibu wa chama
wa kuhakikisha uongozi wake unasimamiwa kwa uwazi na uwajibikaji.
Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga Mwalimu Mathias
Balele imewakumbusha walimu kuhusu wajibu wao wa kufuata maadili ya kazi,
sheria za nchi, katiba na kanuni za chama.
Mwalimu Balele amesema ni muhimu walimu kuendelea kushirikiana kwa pamoja ili kuimarisha
mshikamano wao kwa manufaa ya chama na wanachama wake.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi
CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Mhe. Anord Makombe amewaasa walimu hao kujiepusha
na makundi baada ya uchaguzi huo ambapo amewahimiza kuendelea kuwa wamoja ili
kufikia malengo yao.
Mkutano huu wa CWT Wilaya ya Shinyanga hufanyika
kila baada ya miaka miwili na unatoa fursa kwa walimu kujadili changamoto zao
na kutafuta suluhisho kwa pamoja.
Kauli mbiu ya CWT ni: WAJIBU NA HAKI.
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili
Julius Mtatiro, akizungumza katika mkutano wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga leo Machi 21, 2025.
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili
Julius Mtatiro, akizungumza katika mkutano wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga leo Machi 21, 2025.
Katibu wa CWT Wilaya ya Shinyanga, Rose Mboneko,
akisoma risala kwa mgeni rasmi, leo Ijumaa Machi 21, 2025.
Katibu wa CWT Wilaya ya Shinyanga, Rose Mboneko,
akisoma risala kwa mgeni rasmi, leo Ijumaa Machi 21, 2025.
Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga Mwalimu Mathias
Balele akizungumza kwenye mkutano huo leo Machi 21, 2025.
Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga Mwalimu Mathias
Balele akizungumza kwenye mkutano huo leo Machi 21, 2025.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya
Shinyanga mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza kwenye mkutano mkuu wa CWT
Wilaya ya Shinyanga leo Machi 21, 2025.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza kwenye mkutano mkuu wa CWT Wilaya ya Shinyanga leo Machi 21, 2025.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya
Shinyanga ukiendelea leo Machi 21, 2025 katika ukumbi wa mikutano SHYCOM.
Post a Comment