Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, akizungumza leo Machi 29, 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, leo
Machi 29, 2025 amefuturisha viongozi wa serikali, dini, siasa, makundi
mbalimbali ya watoto wenye uhitaji, na wananchi kwa ujumla.
Katika hafla hiyo, Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga,
Ismail Makusanya, ameongoza dua maalum kwa ajili ya kumuombea Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili Mungu aendelee kumlinda,
kumtangulia na kumuepusha na mabaya katika utekelezaji wa majukumu yake ya
uongozi.
Dua hiyo pia imehusisha maombi ya kuendelea
kudumisha amani, utulivu, na usalama nchini, pamoja na kuombea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ufanyike kwa
amani, na viongozi waadilifu wapate nafasi ya kuhudumu katika majimbo na kata
mbalimbali kwa mujibu wa katiba.
Aidha, Sheikh Makusanya ametumia nafasi hiyo
kumuombea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, pamoja na ustawi wa
mkoa huo kwa ujumla huku akimpongeza kwa jitihada zake katika kuwatumikia
wananchi na kuhakikisha maendeleo yanaendelea kuimarika.
Akizungumza katika hafla hiyo, RC Macha amewashukuru
wafanyabiashara wa Shinyanga kwa kuitikia wito wake wa kuhakikisha bei za
vyakula hazipandi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
"Mwaka huu tumeshuhudia tofauti
kubwa ukilinganisha na miaka mingine, kwani bei za vyakula hazijabadilika
kabisa. Mimi pamoja na wakuu wa wilaya tumefuatilia kwa umakini na tumeridhika
na hali hii," amesema RC Macha
Pia amewapongeza wanasiasa wa mkoa wa Shinyanga kwa
kuzingatia makubaliano ya kutofanya futari za kisiasa kipindi chote cha
Ramadhani, akiwataka waendelee kuzingatia utulivu na mshikamano kuelekea
uchaguzi mkuu wa 2025.
Kuhusu sikukuu ya Eid, RC Macha amewatakia Waislamu
na wananchi wote sherehe njema, huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha usalama.
"Serikali imejiandaa kuhakikisha
kwamba amani na usalama vinakuwepo, lakini ni jukumu la wazazi pia kuwa makini
na watoto wao wasizurure hovyo katika maeneo ya sherehe,"
amesema Macha
Aidha, amewaonya wafanyabiashara wanaotumia sikukuu
kuuza vinywaji vilivyoisha muda wa matumizi, akisema hatua kali zitachukuliwa
kwa watakaobainika.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Mboni Mhita, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Peter Masindi, viongozi wa vyama vya siasa, wakurugenzi wa Halmashauri, na watumishi wa serikali kutoka Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, akizungumza
leo Machi 29, 2025.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya,
akiongoza dua maalum kwa ajili ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Machi 29, 2025 wakati wa hafla ya
futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya,
akiongoza dua maalum kwa ajili ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Machi 29, 2025 wakati wa hafla ya
futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Hafla ya futari ambayo imeandaliwa na Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ikiendelea leo Machi 29, 2025.
Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa dini leo Machi 29, 2025.
Post a Comment