" SERIKALI YAJIIMARISHA KUTOA HUDUMA KIDIGITALI

SERIKALI YAJIIMARISHA KUTOA HUDUMA KIDIGITALI

 

WAZIRI  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene,akizungumza  wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika  Machi 3,2025 jijini Dodoma.

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deus Sangu ,akizungumza wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika Machi 3,2025 jijini Dodoma.

 

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (hayupo pichani), wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika  Machi 3,2025 jijini Dodoma.

 

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (hayupo pichani), wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika  Machi 3,2025 jijini Dodoma.

 

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (hayupo pichani), wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika  Machi 3,2025 jijini Dodoma.

Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya kilichofanyika Machi 3,2025 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WAZIRI  wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene,amesema Serikali  imeendelea kuboresha mifumo ya kiutawala na usimamizi wa Rasilimaliwatu ya kidijitali ili kurahisisha utendaji kazi na kuboresha utoaji wa huduma katika Utumishi wa Umma.

Waziri Simbachawene ameyasema hayo  Machi 3,2025 jijini Dodoma wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Serikali zinazojitegemea,Watendaji Wakuu wa Wakala wa Serikali,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma,Wakurugenzi wa Majiji,Manispaa na Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya.

Amesema Mifumo hiyo inajumuisha Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara, Mfumo wa Huduma kwa Watumishi wa Umma (ess) wenye madirisha ya e- Utendaji Kazi, e-Uhamisho, e-Mikopo, e-Likizo na e- Salary slip; Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Watumishi (HR Assesment); Masjala Mtandao (e-office); Mfumo wa barua pepe wa Serikali (GMS); e-vibali mbadala; Mfumo wa Ajira (Ajira Portal) na Mfumo wa Ushughulikiaji wa Mrejesho wa Wananchi (e-Mrejesho).

“Mifumo hiyo inaendelea kuleta mageuzi ya kiutendaji na utoaji wa huduma wenye lengo la kumfikia na kumhudumia mwananchi kwa haraka, gharama nafuu na kwa ufanisi wa hali ya juu. Mkiwa viongozi mnatarajiwa kuwa vinara katika kuhimiza matumizi ya mifumo mbalimbali ya TEHAMA katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali.”amesema Mhe.Simbachawene

Aidha amesema Mifumo hiyo  imeendelea kusaidia kutatua kero za Watumishi wa Umma na Wananchi kwa kuongeza uwazi na uwajibikaji wa Watendaji kwa wapokea huduma.

Amesema kuwa baadhi ya kero zilizotatuliwa kupitia Mifumo hiyo ni pamoja na kuwezesha Mamlaka za juu za nchi kufahamu hali ya utendaji kazi wa watumishi wa Umma na kuchukua hatua stahiki; kubaini mahitaji halisi ya watumishi katika Utumishi wa Umma; kushughulikia hamisho za watumishi kwa wakati na kudhibiti udanganyifu katika michakato ya uhamisho na ajira.

Ametaja kero nyingine zilizotatuliwa ni kufanya msawazo wa watumishi ndani na nje ya taasisi;, kuboresha ufanisi wa utendaji kazi na kuwezesha wapokea huduma kufuatilia utatuzi wa malalamiko kimtandao badala ya kusafiri umbali mrefu kwenda katika Vituo vinavyotoa huduma hivyo kupunguza gharama za watumishi wa Umma na wananchi katika kufuatilia hoja mbalimbali katika Ofisi za Umma.

Katika hatua nyingune  Mhe. Simbachawene,amekemea tabia ya baadhi ya Wakuu wa Taasisi za Umma nchini  wanaokataa watumishi wanaopangiwa majukumu katika maenee yao ya kwa mujibu wa sheria.
Amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeendelea kupokea malalamiko ya watumishi wanaokataliwa kupokelewa katika vituo wanavyohamishiwa au kuajiriwa.
“Siku za hivi karibuni, kuna mambo yemejitokeza ambayo sio ya kawaida na ni mapya kabisa katika utumishi wa umma.  Baadhi ya mambo hayo ni kwa Waajiri kuchagua aina ya watu wa kufanya nao kazi, kutopokea, kukataa na kuficha barua zenye maelekezo mahsusi ikiwemo barua za uhamisho (kuhamia na kuhama).”

Hata hivyo amesema kuwa  ndoa nyingi za watumishi wa umma zinakufa kutokana na wenza kukaa mbalimbali na kwamba wiki ijayo vitatolewa vibali zaidi ya 200 ili wasogezwe na familia zao.

  “Wapo watumishi ambao tangu ameanza kazi ndoa ina miaka 20 hajawahi kukaa na mume wake kwa zaidi ya mwezi mmoja, wewe Mkurugenzi hasa wa Halmashauri unamzuia huyu kutekeleza ombi lake la uhamisho, wewe unajua kabisa amekaa miaka 20 pale, hata anapokaribia kustaafu busara zikuongoze inahitajika huruma naye akajenge familia yake.”amesema Mhe.Simbachawene
Amesema amezungumza hilo mara nyingi kwa kuwa amebeba uhusika wa mzazi na kwamba binti anapokaa mbali na mume wake inaathiri hadi malezi ya watoto.
“Kuna mwingine anaona anakaribia kustaafu anaona kikokotoo chake kidogo anaomba ahamishwe karibu na nyumbani, hiyo busara haikupati unaona upo sawa, niwaombe mtumie busara kwenye hili,”amesema.
Ameomba waongozwe na busara kwenye suala la uhamisho kwa kuwa wataokoa mambo mengi kwenye jamii na taifa kwa ujumla.
“Tumejipanga sisi tutatoa wale ambao mchujo umekamilika kama zaidi ya 200, wiki ijayo muwasiliane na TAMISEMI mnapopokea ajira mpya mna nafasi ya kuziba mapengo ya uhamisho wa watumishi ambao watakuwa wamekwenda kusogea na familia zao lakini takribani 20,000 mmekaa nazo, nawaomba mtumie busara muokoe ustawi wa familia hizi,”amesema.

Pia amesema kuwa Jumatatu ya wiki ijayo (Machi,10, 2025) Mawaziri watatu watakutana na Umoja wa Walimu wasio na ajira Tanzania (NETO) kwa ajili kujadiliana nao.

Naye, Naibu Waziri, Ofisi hiyo, Deus Sangu, amesema amejaribu kufuatilia na kubaini baadhi ya malalamiko ni uzembe na wengine kudai limekwama Utumishi au TAMISEMI jambo ambalo si kweli.

Alieleza kuwa mamlaka za ajira zina malimbikizo ya mishahara na sehemu kubwa baadhi wametumia kama ni sehemu ya biashara kwamba mtumishi ambaye hatoi chochote jambo lake halishughulikiwi.

Pia, alisema baadhi ya waajiri kutowapa mafunzo elekezi watumishi wapya jambo ambalo linahatarisha utumishi wa umma na inasababisha wingi wa mashauri ya kinidhamu.

Awali, Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Juma Mkomi, amesema kuwa kupitia tathmini mbalimbali inaonesha bado kuna changamoto mbalimbali za kiutendaji katika masuala ya utawala na usimamizi wa rasilimali watu katika utumishi wa umma kutokana na kutozingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo.

“Hali hii imesababisha kushuka kwa hali ya utendaji kazi kwa watumishi na hivyo kuchelewesha utoaji huduma kwa wananchi au kutoa huduma kwa viwango visivyoridhisha,”amesema

Post a Comment

Previous Post Next Post