Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya,
amewataka waumini wa dini ya Kiislamu kuendelea kuzingatia misingi ya dini kwa
kutenda mambo mema kama walivyofanya katika mfungo wa mwezi mtukufu wa
Ramadhani.
Sheikh Makusanya ametoa wito huo leo baada ya Eid - alfitr iliyofanyika katika Uwanja wa Sabasaba Kambarage, Mjini Shinyanga.
Ametoa rai kwa waumini kusherehekea Sikukuu ya Idd
kwa amani na utulivu huku akiwahimiza kujitolea kwa watu wenye uhitaji, hususan
katika siku hii muhimu.
Katika hotuba yake, Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga,
Soud Kategile, amewakumbusha waumini kuhusu umuhimu wa kushiriki kikamilifu
katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo amehimiza kuchagua viongozi bora na
kuepuka vitendo vya rushwa katika kipindi hicho.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, akiongoza
ibada ya swala ya Eid Al Fitr leo Machi 31, 2025 katika uwanja wa Sabasaba
Kambarage Mjini Shinyanga.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, akiongoza
ibada ya swala ya Eid Al Fitr leo Machi 31, 2025 katika uwanja wa Sabasaba
Kambarage Mjini Shinyanga.
Post a Comment