Mgeni rasmi, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma, akizungumza
katika maadhimisho ya siku ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu Mkoani
Shinyanga leo Machi 1, 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii
Tanzania (SMAUJATA), Idara ya Wenye Ulemavu, imeadhimisha siku ya Wanawake na
Wanawake wenye ulemavu Mkoani Shinyanga
kwa lengo la kusisitiza mchango wa wanawake wenye ulemavu katika
maendeleo ya jamii na kupambana na changamoto wanazokutana nazo.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni Waziri wa
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,
Mhe. Riziki Pembe Juma, ambapo amepongeza wanawake wenye ulemavu kwa bidii yao
katika kuchangia maendeleo ya jamii na kuwataka wadau mbalimbali kushirikiana
kuhakikisha kundi hilo linapata nafasi sawa katika sekta zote.
"Siku
ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutambua mchango wa wanawake wote, wakiwemo
wenye ulemavu, katika maendeleo ya taifa. Ni jukumu letu kuhakikisha wanapata
haki zao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi,"
amesema Mhe. Riziki.
Amepongeza juhudi za wanawake wenye
ulemavu katika kuchangia maendeleo ya jamii licha ya changamoto wanazokumbana
nazo.
"Siku ya Wanawake Duniani ni alama muhimu ya kutambua
mchango wa wanawake wote, bila kujali hali zao. Tunapaswa kuhakikisha kuwa
wanawake wenye ulemavu wanapata nafasi sawa katika elimu, ajira na uongozi, ili
wawe sehemu ya maendeleo ya nchi," amesema.
Ameongeza kuwa serikali inaendelea
kuweka mikakati ya kuboresha huduma za jamii kwa wanawake wote, ikiwemo
upatikanaji wa elimu, huduma za afya na maji safi, ili kuhakikisha wanapata
mazingira bora ya maisha.
Amewahimiza wanawake kujikita katika malezi bora ya watoto wao, kwani wao ndio viongozi wa kesho huku akisisitiza kutumia nafasi waliyonayo kuhamasisha vijana kuhusu umuhimu wa kusimamia misingi ya maadili, ili kujenga kizazi chenye uwajibikaji.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa SMAUJATA Taifa,
Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu, amesema kuwa SMAUJATA imeanzishwa ili kuchochea
shughuli za maendeleo na ustawi wa jamii, huku akibainisha kuwa SMAUJATA
ilizinduliwa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi
Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, mnamo Juni 16, 2022.
"Dira
ya SMAUJATA ni kuwa na taifa lenye kizazi huru chenye haki na usawa
kitakachoweza kujitegemea na kuzitambua fursa na kutumia ujuzi, maarifa na
vipaji katika kujenga jamii yenye maendeleo endelevu," amesema
Bulugu.
Akisoma risala Katibu wa Idara ya Wenye Ulemavu
SMAUJATA Taifa, Imani Axwesso, ambaye ameainisha changamoto zinazowakabili
wanawake wenye ulemavu, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ajira, mitaji ya
biashara, mikopo, na nafasi za uongozi.
"Jamii
inapaswa kuhakikisha kuwa mwanamke mwenye ulemavu anashirikishwa kikamilifu
katika nafasi mbalimbali za kimaendeleo ili aweze kujitegemea, lakini pia
ashiriki katika maamuzi muhimu ya uongozi,"
amesema Axwesso.
Ametaja changamoto zinazowakabili wanawake wenye
ulemavu ikiwemo ukatili wa kijinsia, unyanyapaa, na ubaguzi katika jamii huku
akihimiza serikali na wadau wa maendeleo
kuweka mikakati madhubuti ya kuwawezesha kiuchumi na kuhakikisha wanapata
huduma bora za elimu na afya.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha,
ameipongeza SMAUJATA kwa juhudi zake za kupambana na ukatili dhidi ya wanawake
wenye ulemavu, akisema kuwa juhudi hizo zimechangia kupunguza matukio ya
ukatili katika mkoa huo.
Maadhimisho ya mwaka huu yamebebwa na kauli mbiu:
"WANAWAKE NA WASICHANA 2025 TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI."
Kauli mbiu hii inalenga kuhamasisha jamii kutambua uwezo wa wanawake wenye
ulemavu na kuwajumuisha katika ajira, elimu na fursa nyingine za maendeleo.
Mgeni rasmi, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma, akizungumza
katika maadhimisho ya siku ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu Mkoani
Shinyanga leo Machi 1, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha,
akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu
Mkoani Shinyanga leo Machi 1, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha,
akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu
Mkoani Shinyanga leo Machi 1, 2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Taifa, Shujaa Sospeter Mosewe
Bulugu, akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Taifa, Shujaa Sospeter Mosewe
Bulugu, akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Taifa, Shujaa Sospeter Mosewe
Bulugu, akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Taifa, Shujaa Sospeter Mosewe
Bulugu, akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Katibu wa Idara ya Wenye Ulemavu SMAUJATA Taifa, Imani Axwesso, akisoma risala kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1, 2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Bi. Nabila
Kisendi akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Bi. Nabila
Kisendi akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Wanawake na Wanawake wenye
ulemavu Mkoani Shinyanga leo Machi 1,
2025.
Post a Comment