" CHADEMA KANDA YA SERENGETI YALAANI KUFUNGWA KWA TUNDU LISSU, YASISITIZA MSIMAMO WA “NO REFORM, NO ELECTION”

CHADEMA KANDA YA SERENGETI YALAANI KUFUNGWA KWA TUNDU LISSU, YASISITIZA MSIMAMO WA “NO REFORM, NO ELECTION”

Na Mapuli Kitina Misalaba

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Serengeti leo Aprili 16, 2025 kimetoa tamko mbele ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga, kufuatia kikao cha siku tatu cha kamati tendaji ya kanda hiyo kilichofanyika mjini Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Serengeti, Lucas Ngoto, amesema kikao hicho kimepitisha maazimio mbalimbali, huku kikitoa msimamo thabiti wa chama hicho.

Kitendo cha serikali kumfungulia kesi ya uhaini Tundu Lissu ambaye ni mwenyekiti wetu wa CHADEMA Taifa tunakichukulia kama ni hofu ya uchaguzi. Tunalilaani vikali tukio hilo na tunaitaka serikali ya Chama cha Mapinduzi imwachie mwenyekiti wetu mara moja,” amesema Ngoto.

Ameongeza kuwa kuanzia sasa, kanda ya Serengeti itakuwa na ajenda mbili kuu kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Ninawaasa wanachama wa CHADEMA kanda ya Serengeti na Watanzania kwa ujumla kuwa ajenda yetu ya kwanza itaendelea kuwa ‘No Reform, No Election’, lakini kuanzia leo tunaitangaza rasmi ajenda yetu ya pili kuwa ‘Free Tundu Lissu’. Serikali ya CCM wasidhani kutufunga mikono, tutasimamia madai yetu hadi mwisho,” amesema.

Viongozi wa mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga waliokuwepo katika kikao hicho pia wameeleza kuunga mkono jitihada za chama hicho katika kudai mabadiliko ya msingi ya mfumo wa uchaguzi, wakisema kuwa wako tayari kushiriki kikamilifu katika kampeni za kuhamasisha wananchi kudai haki zao za kidemokrasia.

Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Serengeti, Lucas Ngoto, akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 16, 2025.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post