FISTON MAYELE aliomba alipwe mshahara wa dola milioni 1 sawa na [bilioni 2.6] Kwa mwaka ili ajiunge na klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini mwaka 2024.
Mayele ambae tangu amejiunga na Pyramids akitokea Yanga, amekuwa wa moto sana na amefanikiwa kuisaidia klabu hiyo kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Misri.
Mbali na hapo Mayele ameisaidia Pyramids kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika huku akifunga mabao sita [6] hadi sasa katika mechi tisa [9] alizocheza.
Pia Mayele alikuwa mfungaji bora namba mbili [2] katika Ligi Kuu ya Misri msimu wa 2023/24.
Unafikiri Aziz Ki akiondoka Yanga ataweza kuendelea kuwa bora kama alivyo Mayele??????
Post a Comment