Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala
Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa
Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa
wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 imezindua rasmi wiki ya wazazi kwa kufanya
shughuli mbalimbali zikiwemo kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, kupanda
miti na kufanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Sekondari
Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Mwenyekiti wa CCM
Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, ambaye pamoja na kutoa hotuba ya
kuhimiza malezi bora, ushiriki wa wazazi katika maendeleo na mwelekeo wa chama
kuelekea uchaguzi mkuu, ametembelea shule hiyo na kukagua miradi iliyotekelezwa
kwa kipindi cha miaka mitano.
Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara, Mhe.
Mlolwa ameipongeza Jumuiya ya Wazazi kwa kuandaa maadhimisho hayo muhimu ambayo
amesema yanadhihirisha namna wazazi wanavyoshiriki kikamilifu katika kuimarisha
chama na jamii kwa ujumla.
“Jumuiya
ya wazazi imeendelea kuwa nguzo muhimu ndani ya CCM, si tu kwa ushauri bali pia
kwa kukemea maovu na kusimamia maadili,” amesema Mlolwa.
Aidha, amempongeza Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa
wa Shinyanga, John Siagi, kwa kuongoza vyema jumuiya hiyo na kuifanya kuwa
mfano wa kuigwa katika mkoa.
Mlolwa ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa utekelezaji mzuri wa Ilani
ya CCM akibainisha kuwa mkoa wa Shinyanga umepokea miradi mingi ya maendeleo
katika kila kata na kijiji, jambo ambalo limechochea ustawi wa wananchi
kiuchumi na kijamii.
Amesema kuwa katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka
2025, CCM Mkoa wa Shinyanga itahakikisha mgombea urais Dkt. Samia Suluhu Hassan
na mgombea mwenza wake Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi wanashinda kwa kishindo,
huku akisisitiza kuwa Shinyanga itaibuka kinara wa kura za ndiyo kwa nchi
nzima.
Aidha, Mlolwa amewahimiza wananchi kuchagua viongozi
bora wenye maono na uwezo wa kutatua changamoto zao, akionya dhidi ya wagombea
wanaotumia rushwa kutafuta uongozi. “Wajumbe hakikisheni mnapitisha wagombea
wanaokubalika kwa wananchi. CCM haitatoa jina la mgombea anayekubalika”.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi
Mkoa wa Shinyanga, John Siagi, amesema tayari wameandaa mpango kazi kuelekea
uchaguzi mkuu wenye lengo la kuhakikisha CCM inapata ushindi wa kishindo.
Pia amewahimiza wazazi kutumia wiki hiyo kutoa
taarifa za vitendo vya ukatili wa watoto ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Siagi amekemea mmomonyoko wa maadili miongoni mwa
watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwalea watoto katika maadili ya
kitanzania. “Tukiwalea watoto wetu katika misingi bora ya maadili tutakuwa na
taifa la watu wasomi, waadilifu na wenye kujali utu,” amesema Siagi.
Katika hatua nyingine ya uzinduzi huo, Mhe. Mabala
Mlolwa ametembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika shule ya sekondari
Bunambiyu ambapo Mkuu wa shule hiyo, Mzee Matata Joel, ameeleza kuwa serikali
kupitia awamu ya sita imetoa zaidi ya shilingi milioni 166.4 katika kipindi cha
miaka mitano.
Kwa mujibu wa Mzee Matata, fedha hizo zimetumika
kujenga vyumba vya madarasa, ofisi, pamoja na matundu ya vyoo ambapo hadi sasa
zaidi ya shilingi milioni 165.8 zimetumika kwa mafanikio makubwa.
Baada ya ukaguzi huo, viongozi wa CCM wakiongozwa na
Mhe. Mlolwa walipanda miti katika eneo la shule hiyo ikiwa ni ishara ya
utunzaji wa mazingira na kuhamasisha jamii katika suala la mazingira.
Viongozi wengine walioshiriki katika uzinduzi huo ni
pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Odilia Batimayo; Katibu wa Siasa,
Uenezi na Mafunzo, Richard Masele; Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga, Mhe.
Anord Makombe, pamoja na viongozi wengine wa chama na jumuiya zake.
Maadhimisho ya wiki ya wazazi ngazi ya mkoa
yanaendelea kwa kutoa elimu kwa wazazi juu ya malezi bora, afya, elimu,
maadili, pamoja na kujadili masuala muhimu ya maendeleo ya jamii.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala
Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa
Shinyanga leo Aprili 9, 2025.


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala
Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa
Shinyanga leo Aprili 9, 2025.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John
Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John
Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John
Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Regina Ndulu akisoma historia ya jumuiya hiyo.
Post a Comment