Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu mpya wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda, Jimotoli Jilala Maduka, ameanza rasmi majukumu
yake katika Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi, baada ya kuteuliwa hivi karibuni
akitokea kwenye Jumuiya hiyo mkoani Shinyanga.
Mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya CCM Mkoa wa
Katavi kwa ajili ya kujitambulisha, Katibu huyo amepokelewa kwa bashasha na
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndugu Kinyonto, kwa niaba ya
Katibu wa CCM Mkoa huo. Ndugu Kinyonto amemkaribisha rasmi na kumhakikishia
ushirikiano wa dhati katika kuhakikisha kazi za chama zinafanyika kwa weledi na
tija.
Aidha, Maafisa TEHAMA wa CCM Wilaya ya Mpanda pia
wamemkaribisha Katibu huyo kwa furaha na hamasa kubwa, wakieleza kuwa wapo
tayari kushirikiana naye kuhakikisha wanachama wa Jumuiya ya Wazazi
wanasajiliwa kwa usahihi kupitia mifumo ya kisasa ya chama.

Katibu mpya wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda, Jimotoli Jilala Maduka akipokelewa kwa
bashasha na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Katavi, Ndugu Kinyonto,
kwa niaba ya Katibu wa CCM Mkoa huo leo Aprili 17, 2025.

Katibu mpya wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda, Jimotoli Jilala Maduka akiwa kwenye picha ya
pamoja na Maafisa TEHAMA wa CCM Wilaya ya Mpanda leo Aprili 17, 2025.


Post a Comment