NA ANTHONY SOLLO MBOGWE.
Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya
Mbogwe Mkoani Geita chini ya Mwenyekiti wake Mh Khalima Hassan Chembemoyo
imeadhimisha Siku ya Wazazi kwa kutambua mchango mkubwa kutoka kwa wanachama wa
Jumuiya hiyo.
Akihutubia wanachama wa Jumuiya hiyo,Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Wazazi Mh Khalima Hassan Chembemoyo amewataka Viongozi wa Jumuiya hiyo
kutafuta takwimu za Watoto wasioenda Shule ili zipelekwe kwa Mkuu wa Wilaya ili
zifanyiwe kazi ikiwa ni mkakati wa kukabiliana na Adui ujinga katika Wilaya
hiyo na kuipeleka mbele Elimu.
Maadhimisho hayo yalifanyika katika viwanja vya Hospitali ya
Wilaya ya Mbogwe,ambapo viongozi mbalimbali wa Jumuiya hiyo iliyoko chini ya
Chama cha Mapinduzi CCM,pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali Mkoani
Geita,walikusanyika kuadhimisha siku hiyo.
Pamoja na kusherehekea Viongozi hao walisisitiza kuwa moja
ya majukumu ya Jumuiya hiyo ni kutambua jukumu la wazazi katika Malezi, Elimu,
na Ustawi wa Watoto.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wazazi Wilaya ya Mbogwe ,Mh Khalima Hassan Chembemoyo,alisema kuwa wazazi ni
nguzo muhimu katika kuhakikisha mafanikio ya familia na Taifa kwa ujumla.
“Wazazi ndiyo wanaotoa malezi bora na kuwekeza katika watoto
wetu,hivyo kuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa jamii katika siku hii ya
leo,tunawatambua na kuwashukuru kwa juhudi zao zisizo na kifani,”alisema
Chembemoyo.
Aidha, Mwenyekiti huyo aliwahimiza wazazi kuendelea kuwa na
ushirikiano katika kuleta maendeleo ya familia na taifa, huku wakizingatia
maadili ya kitaifa na kukumbatia mabadiliko ya kijamii na kiuchumi
yanayoendelea.
Aliongeza kuwa Jumuiya ya Wazazi itaendelea kutoa elimu kwa
wazazi kuhusu wajibu wao katika kuleta mabadiliko chanya kwa watoto na jamii
kwa ujumla.
Wakati huohuo, Viongozi walisisitiza umoja na mshikamano wa
wazazi,huku wakielezea furaha yao ya kuwa sehemu ya familia kubwa ya CCM ambapo
Katika tukio hilo,Mgeni rasmi alikata Keki kama ishara ya Upendo kwa
wanajumuiya hiyo
Maadhimisho ya Siku ya Wazazi yanakuja ikiwa ni sehemu ya
juhudi za Jumuiya ya Wazazi ya CCM kuhimiza ushirikiano na kuendelea kuchangia
katika maendeleo ya taifa la Tanzania.
Pamoja na mambo mengine Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo
Comrade Charles Kazungu Mabeyo ambaye pia ni mjumbe wa baraza la Wazazi Taifa
kutoka Mkoa wa Geita na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita aliongoza
zoezi la kuchangia Damu kwa ajili ya wagonjwa wahitaji wa huduma hiyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya zoezi la upimaji
Afya katika Maadhimisho ya Wiki ya Wazazi Wilaya ya Mbogwe,Mganga Mfawidhi
Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe Dr Lubinza Maziku Messu amewashukuru wajumbe wa
Jumuiya hiyo kwa kuchangia damu huku akiwaomba kujitokeza kwa wingi kushiriki
zoezi la uchangiaji wa Damu maana ni sehemu muhimu ya upendo kwa kuwa kufanya
hivyo ni kuokoa maisha ya watu wengine anasema Dr Lubinza.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe Mh Sakina Mohamed
alisema Wilaya ya Mbogwe iko shwari, Viongozi wanashirikiana katika kutatua
changamoto.
Mkuu huyo wa Wilaya amempongeza Mwenyekiti wa Chama cha
Mapinduzi Wilaya ya Mbogwe Mathias Nyololo kwa usimamizi mzuri wa Ilani ya CCM
na kuwataka wana CCM kuachana na Propaganda zinazofanywa na Wapinzani kwamba
CCM haijafanya kitu.
Mkuu wa Wilaya amesema Rais Dkt Samia ameleta zaidi ya Sh
bil 70 kwa ajili ya Utekelezaji wa Miradi mbalimbali ikiwemo Miundombinu ya
Barabara,ujenzi wa Vituo vya Afya Pamoja na Miradi ya Maji katika Wilaya ya
Mbogwe.
Hata hivyo baada ya shughuli ya kuchangia Damu,Mgeni rasmi aliendesha
Harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa Jumuiya
ya wazazi Wilaya ya Mbogwe ambapo Mgeni alinunua Mabati yenye thamani ya Sh Mil
3,060,000,huku mbao kwa ajili ya kupaua na kumalizia mapambo zikitolewa na
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa mwakilishi wa Mkoa wa Geita Ndugu
Evarist Paschal Gervas aliyechangia zaidi ya Sh Mil 4.
Aidha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mh Khalima Chembemoyo
alitambua wadau waliofanikisha Sherehe hiyo kuwa ni Pamoja na Ndugu Evarist Paschal
Gervas MNEC kuwakilisha Mkoa Geita,Chacha Wambura (WAJA)ambaye ni Mjumbe wa
Halmashauri Kuu CCM Taifa Viti Ishirini Bara,Mkurugenzi wa Loeni Schools Elias
Ndibato,na Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Nicodemus maganga ambaye alichangia Sh
350,000.

Post a Comment