" NYOTA WA TAARAB KHADIJA KOPA NA DR. ROSE SHABOKA WATUA KAHAMA KWA AJILI YA TAMASHA LA MWANAMKE CHUMA, TAZAMA PICHA WAKIZUNGUMZA GOLD FM

NYOTA WA TAARAB KHADIJA KOPA NA DR. ROSE SHABOKA WATUA KAHAMA KWA AJILI YA TAMASHA LA MWANAMKE CHUMA, TAZAMA PICHA WAKIZUNGUMZA GOLD FM

Mwanamuziki mahiri wa taarab nchini Tanzania, Khadija Omary Abdallah Kopa, pamoja na Pastor Dr. Rose Shaboka, wametua rasmi mjini Kahama kwa ajili ya kushiriki kwenye Tamasha la Mwanamke Chuma 2025, linalotarajiwa kufanyika kesho tarehe 12 Aprili katika ukumbi wa Malex Hall.

Khadija Kopa pamoja na Dr. Rose  wameshiriki kipindi maalum kupitia Gold FM, wakitumia fursa hiyo kuzungumza na wananchi wa Kanda ya Ziwa na Watanzania kwa ujumla, wakiwahamasisha kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha hilo linalolenga kumwinua mwanamke katika nyanja mbalimbali za maisha.

Khadija Kopa, anayefahamika kwa sauti yake ya kuvutia na ujumbe mzito wa nyimbo zake, amesema amefurahishwa na tamasha hilo ambapo amewahimiza wakazi wa kanda ya ziwa kujitokeza kwa wingi  ili kushuhudia burudani ya nyimbo zenye ujumbe.

Kwa upande wake, Dr. Rose Shaboka amesisitiza umuhimu wa mwanamke kupewa nafasi sawa katika uongozi, uchumi, elimu na masuala ya kiroho huku akieleza kuwa tamasha hilo ni jukwaa muhimu la kuwakutanisha wanawake wa rika na taaluma mbalimbali ili kupeana maarifa na kuhamasishana.

Tamasha la Mwanamke Chuma mwaka huu linatarajiwa kuwa kubwa zaidi, likihusisha utoaji wa tuzo kwa wanawake waliotoa mchango mkubwa katika jamii kupitia uongozi, ujasiriamali, elimu, afya na harakati za kijamii.

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM), Jokate Mwegelo, huku wageni wengine wa serikali na taasisi binafsi pia wakitarajiwa kuhudhuria.

MISALABA MEDIA tunatarajia kurusha mubashara tamasha hili kupitia channel ya YouTube, kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya kushuhudia tukio hilo muhimu la kumwinua mwanamke wa Kitanzania.

 Meneja wa Gold FM, Faraji Mfinanga akitioa taarifa fupi ya kituo hicho.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post