Katika kutambua na kuthamini mchango wa walimu katika kuinua
kiwango cha taaluma kwa shule za msingi, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
imetoa tuzo na vyeti vya pongezi kwa walimu na shule zilizofanya vizuri zaidi
kwa mwaka 2024. Hafla hii maalum imefanyika leo, Aprili 12, 2025. Katika ukumbi
wa mikutano shule ya sekondari ya wasichana Shinyanga.
Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hizi, Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Mwl. Samson Hango, ameipongeza Manispaa ya shinyanga kwa kuandaa tukio hilo muhimu.Huku akitumia fursa hiyo kuwasihi walimu kuendelee kujituma na kuweka juhudi zaidi katika ufundishaji, ili kusaidia wanafunzi kufikia malengo yao na kutimiza ndoto zao.
“Tuzo hizi ni alama ya kumbukumbu yenye thamani kubwa kwa walimu na shule kwa ujumla. Twendeni tukajitume, tukawe wazalendo – elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa letu,” amesema Mwl. Hango.
Kwa upande wake, Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Merry Maka, amewapongeza walimu kwa juhudi na moyo wa kujitolea katika kuhakikisha watoto wanapata maarifa ya kusoma, kuandika, na kuhesabu, sambamba na kuwaandaa kuwa viongozi bora wa baadaye huku akiwataka walimu kuongeza juhudi zaidi ili kufikia malengo ya ufaulu ya asilimia 95 kwa mwaka wa elimu 2025, ikiwa ni malengo ya idara ya ekimu Msingi manispaa ya Shinyanga.
Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Elias R. Masumbuko, amewapongeza walimu kwa manispaa ya shinyanga kwa moyo wa kujitolea kuwafundisha wanafunzinje na muda wa kazi hali inayochochea kupanda kwa ufaulu kwa kila mwaka.
Kwa mujibu wa takwimu, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeendelea kufanya vizuri kitaaluma: Mwaka 2022: Ufaulu wa jumla ulikuwa 84.68%. Mwaka 202: Ufaulu wa jumla ulikuwa ni 84.25, huku Ufaulu kwa mwaka 2024 ukipanda hadi 88.42%, ikiiweka Manispaa ya Shinyanga katika nafasi ya kwanza kimkoa kati ya Halmashauri sita za Mkoa wa Shinyanga.
Kwa mitihani wa upimaji wa darasa la nne, Manispaaya manispaa ya shinyanga imeendelea kushika nafasi ya pili kimkoa. Kwa mwaka wa tatu mfululizo (2022-2024.
Hafla hii imelenga si tu kutoa pongezi bali pia kuwa chachu ya kuongeza hamasa kwa walimu na shule nyingine kuendelea kufanya vizuri zaidi.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Elias Masumbuko, akizungumza katika hafla hiyo ya utoaji wa tuzo kwa Walimu, shule na wadau mbalimbali waliochochea kuinua kwa ufaulu wa shule za msingi ndani ya manispaa hiyo.
Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Merry Maka, akizungumza katika hafla hiyo ya utoaji wa tuzo kwa Walimu, shule na wadau mbalimbali waliochochea kuinua kwa ufaulu wa shule za msingi ndani ya manispaa hiyo.
Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Mwl. Samson Hango , akizungumza katika hafla hiyo ya utoaji wa tuzo kwa Walimu, shule na wadau mbalimbali waliochochea kuinua kwa ufaulu wa shule za msingi ndani ya manispaa hiyo.
Post a Comment